ARDHI, MIPANGO MIJI, UPIMAJI NA RAMANI
Utangulizi:
Sekta ya Ardhi, Mipango miji, Upimaji na Ramani ipo katika Klasta ya huduma za Mipango ya Ardhi na Uhandisi (Physical Planning and Engineering Support Services). Dhumuni la Sekta hii ni kutoa ushauri wa kitaalam katika huduma za Mipangomiji, Usimamizi na Utawala wa Ardhi, Upimaji wa Ramani kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Halmashauri na wadau wengine katika fani zilizo chini ya Sekta hii.
Watumishi waliopo kwenye sekta hii ni kama ifuatayo: Ndugu S.C Tossi (AAS PPES & TA - Surveying), A.J.Makubha(Land Officer), M.E. Mjema(Town Planner), P.L Mbelle (Technician Survey) na A. I. Kinunda (Technician Cartographer).
II Shughuli zifanywazo na Sekta ya Ardhi,Mipangomiji, Upimaji na Ramani:
Kushauri wadau mbalimbali kuhusu Mipango miji, Huduma za Ardhi, upimaji na ramani katika mkoa wa Ruvuma.
Kupokea na kutafsiri taarifa, sera, sheria na miongozo mbalimbali ya kisekta kuhusu Huduma za Ardhi, Mipango miji, upimaji na ramani na kuzipeleka Halmashauri kwa utekelezaji.
Kufuatilia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Huduma za Ardhi, Mipango miji, Upimaji na Ramani, kwenye Halmashauri za Wilaya na Manispaa mkoani Ruvuma.
Kuchambua na kuunganisha taarifa mbalimbali za utekelezaji za robo mwaka, mwaka za Halmashauri ambazo zinakuwa kama msingi wa maamuzi ya utendaji kazi.
Kukagua mahesabu ya kazi zote za upimaji zilizofanywa na Halmashauri na kuzipeleka Wizara ya Ardhi kwa Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kwa hatua ya uidhinishaji.
Kukagua na kusaini "deed plans" zote zinazotayarishwa na Halmashauri kwa ajili ya maandalizi ya hati.
Kukagua michoro ya Mipangomiji kutoka katika Halmashauri kabla ya kupeleka kwa Mkurugenzi wa Mipango Miji kwa ajili ya kuidhinishwa.
Kutunza nyaraka na kumbukumbu za Usimamizi na Utawala wa Ardhi, Upimaji na Ramani na Mipangomiji.
Kutambua na kuimarisha mipaka ya Kimataifa, Mkoa na Wilaya
TAARIFA ZA MASUALA YA ARDHI, MIPANGOMIJI NA UPIMAJI WA RAMANI MKOANI RUVUMA
NA |
JINA LA HALMASHAURI |
VIWANJA VILIVYOMILIKISHWA |
MIPAKA YA VIJIJI VILIVYOPIMWA |
VYETI VYA ARHI YA VIJIJI VILIVYOANDALIWA |
VIJIJI VILIVYOANDALIWA MPANGO WA MATUMIZI BORA YA ARDHI |
HATIMILIKI ZA KIMILA ZILIZOANDALIWA |
1 |
Manispaa ya Songea |
24,561 |
Hakuna vijiji |
Hakuna vijiji |
Hakuna vijiji |
Haziandaliwi mijini. |
2 |
H/W Songea |
2,163 |
71 |
35 |
14 |
- |
3 |
H/W Tunduru |
6,814 |
118 |
107 |
15 |
- |
4 |
H/W Mbinga |
9,492 |
153 |
5 |
11 |
250 |
5 |
H/W Namtumbo |
7,079 |
59 |
17 |
61 |
6,298 |
JUmla |
50,109 |
401 |
164 |
101 |
6548 |
|