|
KILIMO
Uchumi wa mkoa huu hutegemea zaidi kilimo, hivyo mkazo mkubwa umewekwa katika kuhakikisha kuwa kilimo kinazidi kukua ili kuchangia zaidi katika kuongeza pato la Mtu binafsi na hatimaye kuondokana na umaskini. Jitihada zinazofanyika ni kuhakikisha kuwa fursa nzuri zilizopo katika kilimo kama vile eneo kubwa la ardhi linalofaa kwa kilimo, hali nzuri ya hewa, mabonde mengi yanayofaa kwa umwagiliaji na nguvu kazi iliyopo vinatumika ipasavyo.
Uzalishaji wa Mazao ya chakula na biashara:
Katika msimu wa kilimo 2006/2007 jumla ya Hekta 390,434 zimelimwa kati ya lengo la kulima hekta 517,272 Utekelezaji huo ni sawa na asilimia 75.5 ya lengo. Sababu kubwa ya kutofikia lengo ni matumizi hafifu ya zana za kilimo.
Matarajio ya mavuno kutokana na eneo lililolimwa ni tani 588,794 sawa na asilimia 76 ya lengo la mavuno ya tani 774,661. Sababu za kutofikia lengo ni pamoja:- Mvua nyingi iliyonyesha kupita kiasi: Wastani wa mvua iliyonyesha ulikuwa ni mm 1448. Kiwango hiki kilikuwa ni kingi zaidi ya wastani wa mvua za kawaida (mm 1100) na hivyo kuathiri uzalishaji wa baadhi ya mazao kama Mahindi, Maharage na Tumbaku. Upungufu wa huduma za ugani na matumizi hafifu ya pembejeo.
Mazao ya chakula :
Eneo lililolimwa kwa ajili ya mazao ya chakula ni hekta 314,075 sawa na asilimia 79 ya lengo la kulima hekta 396,098. Matarajio ni kupata tani 553,223 ya mazao mbalimbali; mahindi tani 243,707, mpunga tani 90,359, muhogo tani 132,777 na mazao mengineyo tani 86,380. Hali ya uzalishaji ni kama ilivyoonyeshwa katika jedwali |

Mahindi

Paddy grown under Irrigation
|
Mwenendo wa uzalishaji wa mazao ya chakula 2004/2005 - 2007/2008
Mazao ya chakula |
2004/2005 |
2005/2006 |
2006/2007 |
2007/2008 |
Hekta |
Tani |
Hekta |
Tani |
Hekta |
Tani |
Hekta |
Tani |
Hekta |
Mahindi |
138,932 |
272,963 |
140,764 |
281,594 |
126,987 |
243,707 |
125814 |
255855 |
Mpunga |
53,055 |
102,926 |
55,373 |
101,503 |
50,111 |
90,359 |
46283 |
79528 |
Maharage |
25,394 |
20,693 |
26,015 |
21,172 |
17,738 |
12,494 |
79109 |
139747 |
Muhogo |
94,078 |
166,999 |
95,298 |
170,269 |
81,307 |
132,777 |
18285 |
14878 |
Viazi Vitamu |
18,608 |
42,332 |
16,983 |
54,887 |
15,838 |
50,457 |
18767 |
53428 |
Ulezi |
13,001 |
10,284 |
12,113 |
8,632 |
9,383 |
5,853 |
9344 |
5417 |
Kunde |
16,200 |
12,960 |
16,732 |
13,232 |
10,268 |
8,127 |
18388 |
14716 |
Mtama |
947 |
674 |
961 |
1002 |
321 |
121 |
180 |
121 |
Mengine |
- |
- |
- |
- |
2,122 |
9,328 |
3161 |
13291 |
Jumla |
360,215 |
629,831 |
364,685 |
665,671 |
314,075 |
553,223 |
319,331 |
576,976 |
Next
|
|
Investments Opportunity |
Tourism |
Tele-Communications |
Extra Information
|
|
Copyright © 2007 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, P.O.BOX 74, Songea, TEL: 025 - 2602238/2602256,2602641, FAX: 025-2602144
[Go Home][WebMaster ] |