• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ruvuma Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Sehemu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Huduma za Sheria
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyo kamilika
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Namtumbo

Waziri wa Ujenzi Eng.Kamwele afanya ziara mkoa wa Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: October 10th, 2018

WAZIRI WA UJENZI ARIDHISWA NA UJENZI WA BARABARA MBINGA-MBAMBA-BAY

Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Mhandisi Izack Kamwele ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Mbinga –Mbamba-bay unaoendelea katika eneo la mbamba-bay nangombo na hajaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa daraja la mto Ruhuhu unaounganisha mkoa wa Ruvuma na Njombe.

Aliyasema hayo jana(tarehe 09.10.2018) wakati akiongea na waandishi wa habari katika eneo la chunya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, kwenye kiwanda cha kusaga mawe kwa ajili ya kokoto wakati akikagua ujenzi wa barabara ya Mbinga-Mbamba-bay yenye urefu wa kilomita 67 ambayo ujenzi wake umeanza katika eneo la Mbamba-bay hadi Nangombo na .

Waziri alifafanua kuwa ameridhishwa na ujenzi wa barabara hiyo jinsi unavyoendelea na maandalizi yake na kumtaka mkandarasi afanye kazi kwa juhudi kubwa na maarifa ili kazi iendelee kwa nguvu zote ili kuwapa wananchi fursa ya kuwa na barabara nzuri watakayoitumia katika shughuli zao za kiuchumi.

Aliongeza kuwa tangu asubuhi alikuwa akitembelea miradi inayotekelezwa katika mkoa wa Ruvuma hususani alikagua barabara ya Likuyufusi –mkenda ambayo alisema upembuzi yakinifu ulishafanyika lakini kutokana na ugunduzi wa makaa ya mawe katika eneo la Muhukuru wamelazimika kufanya tena upembuzi huo kwa kuwa magari mengi yenye uzito mkubwa yatapita katika barabara hiyo na barabara ya kitai-lituhi na lituhi-mbamba-bay pamoja na kukagua daraja la mto Ruhuhu linalounganisha mkoa wa Ruvuma na Njombe.

“Ndugu wanahabari nimekuwepo tangu asubuhi nikiwa nakagua miradi ya maendeleo na hii leo nimekagua barabara ya Likuyufusi –Mkenda ,kitai-Lituhi na Lituhi-Mbamba-bay na Mbamba-bay-mbinga kwa kifupi na ujenzi wa barabara ya mbinga-Mbamba-bay kwa kuwa maandalizi yake na mazuri na hata kasi ya ujenzi ni nzuri na inaendelea vizuri Lakini Sijaridhika na ujenzi wa Daraja la mto nimeridhishwa Ruhuhu kwa kuwa Mkandarasi huyo ni Mtanzania lakini hana uwezo wa kujenga lile Daraja.Nimeongea nae mkandarasi anayejenga daraja na sijataka nitoe amri ya kuwachisha kazi lakini nimemshauri aonane na wakala wa barabara Tanroad Mkoa wa Ruvuma ili akabidhi yeye mwenyewe ile kazi ili iweze kukamilika kwa muda wa miezi miwili kwa kuwa kazi iliyobaki siyo kubwa sana.”

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba alimpongeza waziri huyo kwa mikakati ya ujenzi wa barabara hizo na kusema kuwa kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Nyasa anaishukuru sana Serikali ya awamu ya tano kwa kujenga Barabara za huku mpakani mwa Tanzania kwa kuwa barabara ya Lituhi Mbamba-bay iko karibbu mpakani mwa tanzani na malawi upande wa Tanzania hivyo itasaidia sana katika ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa Wilaya ya Nyasa.

Katika hatua nyingine amefurahi kuona rasilimali ya makaa ya mawe iliyopo katika mkoa wa Ruvuma Muhukuru Wilayani Songea pamoja na Ruanda Wilayani Mbinga kwa kuwa ni vichocheo vya ukuaji wa sekta ya Viwanda kwa kuwa Viwanda vingi vinatumia makaa ya mawe na akavitaja viwanda hivyo kuwa ni cha Dangote Mtwara na viwanda vya simenti cha Tanga na Dar es salaam na viwanda vingine vya nchi jirani za Rwanda na Kenya.

IMEANDALIWA NA

NETHO C. SICHALI

AFISA HABARI

NYASA DC

09 Octoba,2018

Matangazo

  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2018 January 24, 2019
  • Kikao cha Maandalizi ya Wiki ya Maonyesho ya Viwanda na Uwekezaji January 23, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi waliofaulu Kidato cha Kwanza Mkoa wa Ruvuma 2019 December 17, 2018
  • Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani December 02, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Watumishi 3 Manispaa ya Songea Wasimamishwa Kazi

    February 17, 2019
  • Watumishi wa Umma Kuweni na Subira Ongezeko la Mishahara - Waziri Mkuu Majaliwa

    February 08, 2019
  • Ufuatiliaji wa Mapato ya Ndani kwenye Halmashauri za Ruvuma

    January 17, 2019
  • Mpokezi ya Waziri Mkuu Ruvuma

    January 03, 2019
  • Angalia zote

Video

MAAGIZO YA MKUU WA MKOA KWA WATENDAJI WAKUU NA WATUMISHI WA SERIKALI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Kurasa Mashuhuru

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Regional Commissioner Office

    Anwani ya Posta: 74 Songea

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: 0252602256

    Barua pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusha
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimili@2017 Ruvuma.Haki zote zimeifadhiwa