Kandokando mwa milima ya Umatengo, katika kijiji cha Kigonsera wilayani Mbinga mkoani Ruvuma, kuna shule ambayo historia yake imevuka mipaka ya elimu na kuwa fahari ya taifa. Shule ya Sekondari ya Wavulana Kigonsera, iliyoanzishwa mwaka 1938 na Shirika la Wabenediktini wa Peramiho, leo ni urithi wa kitaifa na kivutio cha utalii wa kihistoria Tanzania.
Baada ya uhuru, mwaka 1961, serikali iliitaifisha shule hiyo ili kutoa elimu bila ubaguzi wa dini, rangi au kabila, kulingana na sera za elimu na Katiba ya 1977. Kwa zaidi ya miaka 80, Kigonsera wamehitimu wanafunzi 13,266, ambapo asilimia 96 wameendelea na elimu ya juu, ajira na uongozi ndani na nje ya nchi.
Umaarufu wake mkubwa unatokana na kuwazaa viongozi wawili wa juu kabisa nchini: Hayati Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa. Mafanikio haya yameifanya Kigonsera kuwa “makumbusho hai” ya uongozi wa Tanzania.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.