• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC MNDEME awatoa hofu wanafunzi wa kidato cha sita,Mkoa wa Ruvuma hauna corona

Imewekwa kuanzia tarehe: June 4th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewahakikishia usalama wanafunzi wa kidato cha Sita wawapo  shuleni  hususani katika kipindi hiki kigumu cha kupambana na  janga la Corona.

Akizungumza na wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari Kigonsera iliyopo Wilaya ya Mbinga,Mndeme  amesema,Mkoa wa Ruvuma hauna Mgonjwa hata mmoja wa Corona,hata hivyo ametoa rai kwa wanafunzi kuendelea kuchukua tahadhari ya kukabiliana na maambukizi ikiwemo kutumia barokoa,maji na sabuni.

Mndeme amewataka wanafunzi kuongeza bidii na kasi ya kusoma , kutii maelekezo watakayopewa na walimu wao, ili mwaka huu Mkoa wa Ruvuma katika Matokeo ya kidato cha Sita iwe miongoni mwa Mikoa mitatu  itakayofanya vizuri Kitaifa.

“Shule ya Kigonsera ina historia iliyotukuka kitaifa kwa sababu imemtoa Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa,pia imemtoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa hiyo shule hii ina heshima yake’’,alisisitiza.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amewaagiza TARURA kutatua changamoto ya Barabara inayofika shuleni hapo ili  itengenezwe na kupitika mwaka mzima kipindi cha kiangazi na Masika.

Mkuu wa shule ya Sekondari ya Kigonsera Ponsiano Ngunguru amewataja wanafunzi wa Kidato cha sita walioripoti shuleni ni 163 na ambao bado hawajaripoti hadi kufikia Juni 2 mwaka huu ni  199 na kwamba shule hiyo ina jumla ya wanafunzi wa kidato cha sita 362.

Shule ya Sekondari ya Kigonsera ni miongoni mwa shule kongwe za Serikali nchini iliyoanzishwa mwaka 1938.

Wakati huo huo Mkuu wa shule ya sekondari ya Maposeni Dismas Nchimbi  amewataja wanafunzi wa kidato cha sita walioripoti katika shule hiyo hadi kufikia Juni 3 kuwa ni  191 kati yao wavulana 101 na wasichana 90 .Shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 222.

Imeandikwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Habari Mkoa wa Ruvuma

 Juni 3, 2020

Matangazo

  • RATIBA ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 October 14, 2023
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara December 31, 2023
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma September 30, 2023
  • WALIOCHAGULIWA kidato cha kwanza March 31, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI kuendelea kutoa mbolea ya ruzuku

    September 24, 2023
  • PPRA yatangaza kufunga rasmi mfumo wa ununuzi wa TANePs Septemba 30 mwaka huu

    September 23, 2023
  • MKUU wa Mkoa alivyomkabidhi Mkakati wa Utalii Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma

    September 23, 2023
  • CHIFU wa Wangoni alivyokabidhiwa Mkakati wa Utalii Mkoa wa Ruvuma

    September 23, 2023
  • Tazama zote

Video

WAZIRI APONGEZA UWEKEZAJI MKUBWA HALMASHAURI YA MADABA
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: 0252602256

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.