Serikali kupitia TARURA imetenga TSh bilioni 5.2 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kuboresha miundombinu ya barabara wilayani Mbinga, mkoani Ruvuma Hatua hii inayolenga kurahisisha usafirishaji wa mazao na kukuza uchumi wa wananchi.
Akizungumza kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Kisare Makori, alisema uwekezaji huo umeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya usafiri na kilimo, akisisitiza kuwa Mbinga ni “kapu la chakula la Taifa.”
Kupitia TARURA, wilaya hiyo imenufaika na miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa Km 6, stendi mpya ya kisasa Lusaka, na soko jipya la kisasa. Pia, Serikali imeendelea kuweka taa za barabarani kwa ajili ya kuongeza usalama na kupendezesha mji.
Wananchi nao wamepongeza juhudi hizo wakisema taa zimepunguza uhalifu na kuongeza muda wa kufanya biashara.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.