Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imezindua rasmi mpango wa kutoa miche bora ya kahawa kwa wakulima, lengo likiwa kuongeza uzalishaji, kuinua kipato cha wakulima na kuongeza mapato ya Manispaa.
Afisa Ushirika wa Manispaa, Given Malik, amesema mpango huu unashirikisha wadau wakubwa akiwemo TACRI na Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) ili kuhakikisha wakulima wanapata:
✅ Mbegu bora
✅ Madawa ya kisasa
✅ Masoko ya uhakika
“Tunafufua tena kahawa Songea. Wakulima watapata elimu, miche bora, masoko na huduma za ugani. Ushirika ndio nguzo ya mafanikio yao,” – Malik.
Wakulima wa Songea wamepokea mpango huu kwa shangwe, wakiweka matumaini mapya kwamba kahawa itarejea kuwa injini ya maendeleo binafsi, ya Manispaa na ya Taifa
Wakulima wa Ndilimalitembo tayari wameonesha mfano kwa kuanzisha mashamba ya kahawa.
Kahawa ya Songea ni fursa ya kiuchumi, ajira na maendeleo ya jamii. Mpango huu unatarajiwa kuwashawishi wakulima wengi zaidi kuwekeza tena kwenye zao hili la kimkakati.
#Songea #KahawaYaTanzania #KilimoBiashara #Ushirika #Fursa
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.