Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Bw. Crispin Chalamila, amekabidhi mashine mbili za kisasa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songea kwa ajili ya:
Kutengeneza joto kwa watoto njiti
Matibabu ya ugonjwa wa manjano kwa watoto wachanga
Hafla hiyo imefanyika l12 Oktoba 2025, katika viwanja vya hospitali hiyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za TAKUKURU kuunga mkono maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha huduma za afya kwa Watanzania wote .
“Tumechagua Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songea kwa kuwa ni kitovu cha huduma za afya mkoani Ruvuma, hivyo msaada huu utawanufaisha wananchi wengi zaidi,”
— Crispin Chalamila, Mkurugenzi Mkuu – TAKUKURU
Kwa upande wake, Dkt. Regina Hyera, Daktari Bingwa wa magonjwa ya watoto, amesema vifaa hivyo vitawezesha hospitali kutatua changamoto kubwa kwani asilimia 43 ya watoto wanaolazwa ni njiti, na mashine kama Infant Radiant Warmer itasaidia kudhibiti joto la mwili wa watoto hao
Aidha, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Louis Chomboko, ametoa shukrani kwa TAKUKURU kwa mchango huo muhimu unaolenga kuimarisha sekta ya afya, kupunguza vifo vya watoto wachanga, na kuongeza ufanisi wa huduma za afya katika Mkoa wa Ruvuma.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.