Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limekabidhi vitambulisho kwa wakaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi katika kusimamia ubora wa bidhaa za chakula na vipodozi.
Uwasilishaji huo umefanyika kufuatia Kanuni za Viwango na Ushirikiano katika Utekelezaji wa Mamlaka na Majukumu ya mwaka 2021, pamoja na makubaliano rasmi ya ushirikiano yaliyosainiwa kati ya TBS na halmashauri zote nchini Tanzania Bara.
Kupitia makubaliano hayo, TBS imekabidhi baadhi ya majukumu yake kwa halmashauri, ikiwemo ukaguzi na usajili wa majengo ya chakula, ambapo wakaguzi wa halmashauri sasa wanatekeleza majukumu hayo kwa niaba ya TBS. Vitambulisho hivyo maalum vinawapa mamlaka ya kisheria kufanya ukaguzi wa maeneo yote yanayohusiana na biashara ya chakula na vipodozi, ili kuongeza uwazi, uhalali na ufanisi katika utoaji wa huduma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Ndg. Chiza Marando, ameishukuru TBS kwa hatua hiyo, akibainisha kuwa hatua hiyo itaimarisha uwajibikaji wa wakaguzi na kuhakikisha bidhaa zote zinazouzwa katika Wilaya ya Tunduru zinakidhi viwango vya ubora na usalama.
Hatua hii ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia TBS kuhakikisha kuwa viwango vya ubora na usalama wa bidhaa vinazingatiwa katika ngazi zote nchini, kwa manufaa ya afya na ustawi wa wananchi.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.