Timu ya Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa wa Ruvuma ikiongozwa na Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Joel Mbewa Novemba 6.2025 imefanya ufuatiliaji wa miradi minne ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 875 katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea.
Miradi iliyofuatiliwa utekelezaji wake ni ujenzi wa nyumba nne za watumishi katika shule ya sekondari Matetereka wenye gharama ya zaidi ya shilingi milioni 201,ujenzi wa kituo cha walimu katika shule ya msingi Ifugwa Kata ya Lituta wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 51,ujenzi wa vyumba sita vya madarasa,mabweni mawili na matundu 10 ya vyoo katika shule ya sekondari Madaba unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 417 na mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi ya Madaba katika Kata ya Lituta unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 205.
Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo Mbewa amewapongeza wataalam kwa kusimamia miradi hiyo ambapo mingine ikiwa imeanza kutumika ukiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba nne za walimu
Hata hivyo amesisitiza kuongeza kasi ya utekelezaji kwa miradi ambayo bado haijakimilika huku akisisitiza kuzingatia viwango bora katika utekelezaji wa miradi hiyo.
Timu ya Menejimenti mkoa wa Ruvuma leo Novemba 7 bado inaendelea na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Madaba
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.