• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa kahawa Nyasa waipongeza serikali kuboresha bei ya soko la Dunia

Imewekwa kuanzia tarehe: April 22nd, 2025

Wakulima wa zao la kahawa katika Kijiji cha Kingerikiti, Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kusimamia kwa mafanikio bei ya zao hilo katika soko la dunia, kutoka Sh. 3,000 mwaka 2021/2022 hadi Sh. 8,500 kwa kilo moja. Wamesema ongezeko hilo limeleta mafanikio makubwa katika maisha yao na kuchochea ari ya kuendelea na kilimo hicho.

Mkulima Vitus Mapunda amesema awali walikumbwa na changamoto ya bei ndogo ya kahawa huku gharama za uzalishaji zikiwa juu, hali iliyowafanya kuishi maisha magumu licha ya juhudi kubwa mashambani. Hata hivyo, amepongeza Serikali kwa kuboresha hali hiyo kupitia sera madhubuti za kilimo, hasa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Mapunda ameongeza kuwa upatikanaji wa mbolea za ruzuku umechangia ongezeko la uzalishaji kutoka tani nne hadi kufikia tani kumi kwa ekari moja. Hii imetokana na usimamizi mzuri wa Serikali katika kila hatua ya uzalishaji wa kahawa, kuanzia maandalizi ya shamba hadi kuuza mazao sokoni.

Hata hivyo, Mapunda na wakulima wengine wameitaka Serikali kuongeza maafisa ugani katika kila kijiji badala ya kuishia ngazi ya kata, ili wakulima wengi waweze kufikiwa na kuelimishwa kuhusu kilimo bora. Wamesema ukosefu wa elimu hiyo unarudisha nyuma jitihada za kuongeza uzalishaji wa mazao mashambani.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Msingi cha Ushirika wa Kilimo na Masoko Kingerikiti, Fabian Ndunguru, amesema kupitia ushirikiano wa kimataifa, Amcos yao imepata ufadhili kutoka Marekani wa Sh. milioni 588, fedha zitakazotumika kujenga miundombinu muhimu kama maabara ya kahawa, sehemu ya kukaanga na ghala la kuhifadhi mazao. Hii ni hatua kubwa kuelekea kuongeza thamani ya zao hilo na kuongeza kipato cha wakulima.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waridhia miradi yote Tunduru

    May 16, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waangaza Namtumbo

    May 15, 2025
  • AMEUONA Mwenge Songea baada ya miaka 63 ya Uhuru

    May 14, 2025
  • MWENGE wa Uhuru watingisha Manispaa ya Songea,wapitia miradi ya bilioni 1.8

    May 14, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.