Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma Mhe. Peres Magiri, amewahakikishia wananchi kuwa hali ya usalama ni shwari kabisa, hivyo wote wajitokeze kwa amani kupiga kura ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025.
Magiri ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Wilaya, amesema kila raia aliyejiandikisha kwenye daftari la kudumu ana wajibu wa kutumia haki yake ya kidemokrasia kuwachagua viongozi watakaoleta maendeleo endelevu kwa Taifa.
Ameongeza kuwa kupiga kura ni takwa la kisheria lililoainishwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo akawataka mabalozi wa nyumba kumi na viongozi wa mitaa kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi.
Kwa upande wake, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Nyasa, Ausi Mkwanda Limia, amesema maandalizi yote yamekamilika na vituo vya kupigia kura vitakuwa wazi kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni.
“KUPIGA KURA NI HAKI YAKO — JITOKEZE TAREHE 29 OKTOBA 2025.”
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.