Wilaya Tunduru mkoani Ruvuma inaingia kwenye sura mpya ya kilimo baada ya maafisa kilimo kupatiwa mafunzo maalum kuhusu miongozo ya uzalishaji bora—hatua inayolenga kuongeza mavuno, kulinda mazingira na kuimarisha afya ya udongo kwa maendeleo endelevu ya wakulima.
Mafunzo hayo yametolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) yakisisitiza matumizi ya mbinu za kisayansi, zikiwemo utumiaji sahihi wa mbolea na viuatilifu, uchaguzi wa mbegu bora pamoja na uhifadhi salama wa kemikali ili kuongeza tija bila kuathiri mazingira.
Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Ndugu Chiza Marando, amesema wataalamu wa kilimo wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha uzalishaji unaongezeka kwa kuwajengea wakulima uelewa sahihi wa kilimo bora. Pia amewahimiza kutumia kikamilifu zana zilizopo, ikiwemo matrekta, ili kuharakisha mapinduzi ya kilimo wilayani humo.Mafunzo hayo yanatarajiwa kuwa chachu ya mabadiliko kwa sekta ya kilimo Tunduru, yakifungua fursa zaidi za kiuchumi kwa wakulima na kuchangia usalama wa chakula nchini.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.