Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma christina Mndeme ametembelea eneo la Mto Mnywamaji katika Kijiji cha Ruanda wilaya ya Mbinga ambako watumishi watano wa kampuni ya TANCOAL inayochimba madini ya makaa ya mawe kunusurika baada ya gari walilokuwa wanasafiria kusombwa na maji ya mto huo.
Naibu katibu mkuu wa Wizara ya Maliasili na utalii DKT.Aloyce Nzuki amesema serikali inatarajia kurejesha nchini mafuvu 200 ya mashujaa yaliyopo nchini Ujerumani na kwamba mafuvu hayo yafanyiwa maziko up ya na kwa heshima wanayostahili.Alikuwa nazungumza katika kumbukizi ya miaka 113 ya mashujaa wa vita ya Majimaji mjini Songea.
MKOA wa Ruvuma umepanda katika utoaji lishe kutoka asilimia 67 mwaka jana hadi kufikia asilimia 84 mwaka huu Hayo yamebainika katika mkutano wa nusu mwaka wa Ripoti ya tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe ngazi ya mkoa wa Ruvuma.Mkutano huo umeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na kuwashirikisha wakuu wote wa wilaya,makatibu tawala wote,maafisa lishe na wadau wengine wa lishe.
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.