Kikao cha wadau wa maji mkoani Ruvuma kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma christina Mndeme kimepitisha azimio la kuwaondoa wote waliovamia vyanzo vya maji na kuendesha shughuli za kiuchumi ikiwemo Kilimo ili kulinda na kihifadhi vyanzo hivyo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na baadaye.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewaomba viongozi wa Umoja wa makanisa mkoani Ruvuma kufanya maombi maalum ya kuondoa pepo la kuvuta na kulima bangi ili kupunguza madhara makubwa yanayowapata wanaovuta bangi
Mtaalamu Mwandamizi kutoka Mamlaka ya usimamizi wanyamapori Tanzania (TAWA) akiwa na timu ya wataalam amefanya ziara ya kikazi kukagua kisiwa cha Lundo ziwa Nyasa ambapo amesema kisiwa hicho kinafaa kwa Wanyamapori wanaokula Nyasi hivyo TAWA wanaendelea na mchakato wa kuleta wanyama wanaokula nyasi katika kisiwa hicho kwa upande wake Mwekezaji aliyeomba kuwekeza katika kisiwa hicho ameridhishwa na madhari ya kuvutia ndani ya kisiwa hicho hivyo anakusudia kujenga hoteli ya kitalii.
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.